Archive Pages Design$type=blogging

MUBASHARA NDONDO CUP NA AZAM TV.

Kituo cha Televisheni cha Azam kimeingia makubaliano ya mwaka mmoja ya kuonesha mubashara mashindano ya Ndondo hatua ya makundi Mkoa wa Da...

Kituo cha Televisheni cha Azam kimeingia makubaliano ya mwaka mmoja ya kuonesha mubashara mashindano ya Ndondo hatua ya makundi Mkoa wa Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya kutia saini makubaliano hayo jana, Mkurugenzi wa Azam TV, Tido Muhando alisema wameingia makubaliano na Clouds Media ili kuwaonesha watu wasioweza kufika katika viwanja kushuhudia mashindano hayo.

“Tunawaahidi Clouds Media na Watanzania tutafanya kazi nzuri kwani sisi ndio kituo bora kwa urushaji wa matangazo hasa soka hilo halina ubishi,” alisema Tido. Naye Mratibu wa Ndondo Cup, Shafii Dauda aliwashukuru Azam Media kuwa sehemu yao katika kuendesha mashindano hayo kwa miaka minne mfufulizo.

“Lengo la mashindano ni kutengeneza daraja kwa vijana wenye vipaji ili waonekana na wasajiliwe na timu za madaraja ya juu hivyo tunaishukuru Azam Media kuwa sehemu yetu kufanikisha ndoto za vijana,” alisema Shafii.

Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam, Almas Kasongo aliishukuru Azam Media na Clouds Media kwa kusaidia kuendeleza michezo Dar es Salaam. “Tunafurahi kuona soka likichezwa katika mkoa wetu kwani mnasaidia kutekeleza moja ya majukumu yetu hivyo nawaahidi mashindano haya yatasimamiwa kwa weledi mkubwa,” alisema Kasongo.

Droo ya makundi ya mashindano hayo inatarajiwa kuchezeshwa leo katika viwanja vya Escape One, Kinondoni ambapo timu 32 zitakuwa kwenye bakuli moja. Timu hizo ni Vituka FC, Twiga International, Kigoma Kombaini, Stimtosha, Tandavamba, Black Six, Ukwamani, Ndanda Investment, Miami, Mpakani Kombaini na Kibo Kombaini.

Vijana rangers, Goroka FC, Burudani, Polisi DSM College, Faru jeuri, Boom FC, Temeke Market, Temeke Squad, Tabata United, Misosi, Keko Furniture na Buguruni United. Nyingine ni Goms United, Kigogo Kombaini, Wauza matairi, Shelaton, Makuburi, Kibada One, Kauzu FC, Mlalakuwa Rangers na Madiba FC.

COMMENTS

Name

BURUDANI HABARI MAKALA MICHEZO
false
ltr
item
DIMBWI LA HABARI TZ: MUBASHARA NDONDO CUP NA AZAM TV.
MUBASHARA NDONDO CUP NA AZAM TV.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg6qarlnD6Gw3Hrk0ha5Qs6n-v4clgigMjbf4Rr4_Ccw_VBKhyRrZzAM7yBIbF3oTzZzlHk1we9QolDnV6RSzEClEYN4pp1Fhbkh6M1pl5D733pIZ9TpAgIQ-C-vAY-RL9U-UNedSKE7qIX/s1600/ben.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg6qarlnD6Gw3Hrk0ha5Qs6n-v4clgigMjbf4Rr4_Ccw_VBKhyRrZzAM7yBIbF3oTzZzlHk1we9QolDnV6RSzEClEYN4pp1Fhbkh6M1pl5D733pIZ9TpAgIQ-C-vAY-RL9U-UNedSKE7qIX/s72-c/ben.jpg
DIMBWI LA HABARI TZ
https://dimbwilahabari.blogspot.com/2017/06/mubashara-ndondo-cup-na-azam-tv.html
https://dimbwilahabari.blogspot.com/
https://dimbwilahabari.blogspot.com/
https://dimbwilahabari.blogspot.com/2017/06/mubashara-ndondo-cup-na-azam-tv.html
true
8218800783604508792
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago