Archive Pages Design$type=blogging

Uhuru na Lowassa waomba Wakenya kuvumiliana 15 Julai 2017 ...

Uhuru na Lowassa waomba Wakenya kuvumiliana

  • 15 Julai 2017
 
Kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Edward Lowassa 

Aliyekuwa waziri mkuu nchini Tanzania na mgombea wa urais katika chama cha upinzani Chadema katika uchaguzi uliopita Edward Lowassa amewataka Wakenya kuvumiliana wakati huu ambapo taifa hilo linakaribia uchaguzi.

Akizungumza nchini Kenya katika mazishi ya aliyekuwa waziri wa usalama nchini humo marehemu Joseph Nkaiserry, Lowassa amesema kuwa kenya inapaswa kujifunza kutoka kwa machafuko ya uchaguzi ya mwaka 2007.

Matamshi yake yaliungwa mkono na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta aliyewataka wafuasi wake na wale wa kiongizi wa upinzani Raila Odinga kuvumiliana.


Uhuru alisema kuwa hakuna haja ya kupakana tope za matusi akiongezea kuwa matusi hayasaidii.

''Sisi sote ni Wakenya , hatuna taifa jingine la kujenga baada ya uchaguzi ,tunaomba amani, amani amani'', alisema rais Uhuru Kenyatta.

Matamshi ya Uhuru na Lowassa yanajiri wakati ambapo wafuasi wa upinzani na wale wanaounga mkono serikali wamekuwa wakiwazomea viongozi wanaotoka pande pinzani katika mikutano ya kampeni na hata kusababisha mikutano hiyo kusitishwa.

Lowassa amesema kuwa Kenya ni tegemio la kiuchumi katika mataifa ya Afrika mashariki hivyobasi inafaa kuwa mfano kwa kuhakikisha kuwa taifa hili halijiingizi tena katika jinamizi la machafuko yalioonekana miaka 10 iliopita.

''Ombeni musirudi katika mapigano yaliotokea mwaka 2007, Kenya iko mbele kushinda taifa lolote lile Afrika mashariki na tunataka muendelee kusonga mbele.

a

Lowasa alisema kuwa marehemu Nkaissery aliamini sana Umoja wa Afrika mashariki na alijitolea kufanya kazi na akawataka viongozi wengine kuiga mfano wake.

Naye rais Uhuru aliongezea kwamba Kenya na Tanzania ni pacha na zitaendelea kuimarisha ushirikiano wao kwa lengo la kurahisisha biashara na usalama kati ya raia wa mataifa hayo mawili.

Miongoni mwa wale waliohudhuria mkutano huo ni pamoja na kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga na naibu wa rais William Ruto

COMMENTS

Name

BURUDANI HABARI MAKALA MICHEZO
false
ltr
item
DIMBWI LA HABARI TZ
https://ichef.bbci.co.uk/news/320/cpsprodpb/F95A/production/_96943836_edwardlowassa.jpg
DIMBWI LA HABARI TZ
https://dimbwilahabari.blogspot.com/2017/07/uhuru-na-lowassa-waomba-wakenya.html
https://dimbwilahabari.blogspot.com/
https://dimbwilahabari.blogspot.com/
https://dimbwilahabari.blogspot.com/2017/07/uhuru-na-lowassa-waomba-wakenya.html
true
8218800783604508792
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago