post-feature-image
HomeMAKALA

Usikatishwe Tamaa Kwa Kukataliwa Na Dunia.

Usikatishwe Tamaa Kwa Kukataliwa Na Dunia 14JULY2017. Kama upo kwenye mbio sahihi za mafanikio, kati ya kitu ambacho unataki...

Usikatishwe Tamaa Kwa Kukataliwa Na Dunia

14JULY2017.
Kama upo kwenye mbio sahihi za mafanikio, kati ya kitu ambacho unatakiwa kujifunza sana ni kutokukatishwa tamaa na kukataliwa. Upo wakati utakataliwa kwenye biashara yako na kukosa wateja.

Hiyo haitoshi kuna wakati utakataliwa sana kwa kazi unayoomba na pia kuna wakati unaweza kukataliwa na mazingira na kushindwa kuvuna hata kile ulichopanda. Hiyo ni mifano michache kati ya mingi.

Kitu cha kujiuliza kukataliwa kwa namna yoyote kunapotokea kwako, huwa unachukuliaje? Huwa unajiona ni mpumbavu au mjinga au unakuwa unatumia kukataliwa huko kama sababu ya kusonga mbele?

Kwa wengi sina shaka sana kukataliwa kokote kunapotokea, ndani mwao hujisikia vibaya sana kiasi cha kwamba kutokutamani kuendelea tena. Je, hi ndiyo hali ambayo hutokea hata ndani mwako?

Usichokijua wapo watu wengi sana ambao walikataliwa mwanzoni na kazi zao lakini leo ni mabilionea. Sylvester Stalone alimaarufu Rambo alishindwa kupata uzamini wa kutoa filamu yake ya kwanza hadi aliuza mbwa wake.

Naye pia Alexander Graham Bell alipopeleka kwa mara ya kwanza kuiza teknolojia yake ya Simu  kwa Carl Orton ambaye ni mmliki wa Western union aliambiwa kampuni kubwa kama yake haiwezi kununua doli kama hilo.

Hebu jiulize ni kitu gani ambacho alikuwa akiwaza Rambo pale alipoambiwa hawezi kuigiza, au ni kitu gani alichokuwa akifikiri Bell pale alipoambiwa kazi yake ni hovyo na kufananishwa na doli?
Kwa ujasiri na ushujaa, hakuna aliyekata tamaa, waliamua kusonga mbele, leo hii dunia nzima inatumia simu na leo hii wengi wanamfahamu Rambo. Katika mazingira yoyote ulionayo hapo ulipo, usikubali kukatishwa tamaa na kukataliwa, simamia ndoto yako kikamilifu.

Ni kweli kuna wakati utapita katika mazingira magumu na kuonekama kila kitu kimekataa kabisa kwenye maisha, lakini hiyo usichukulie kwamba ndio uhalisia ulivyo. Chukua jukumu la kuendelea kusonga mbele.

Asikuzuie mtu kwa maneno yake, yasikuzuie mazingira yoyote yale, kitu cha msingi usikubali kushindwa kwenye akili yako kwanza, ukishindwa huko na huku nje utakuwa umeshindwa. Kabisa.
Hapo ulipo unajijua vizuri hali uliyonayo, hali hiyo kama huipendi sana amua kuibadili mara moja, kama unaona huoni matokeo ya haraka usikate tamaa, vumulia mambo yatakaa sawa kadri siku zinavyokwenda.
Name

BURUDANI HABARI MAKALA MICHEZO
false
ltr
item
DIMBWI LA HABARI TZ: Usikatishwe Tamaa Kwa Kukataliwa Na Dunia.
Usikatishwe Tamaa Kwa Kukataliwa Na Dunia.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi2w4VsztSYwf0OXaJ8Eaqr-3W9vQ76CltJb8OFZhMITf88Ng5OdSTMPrzJx5AvwK4sUv-C77MjaSwufoxZspHbbM-fD4O8oueIbLof3MGBIdNuDqKyOdOY_CvcvZZ3vQ6UgMLX_AhRG2rd/s640/hopeW.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi2w4VsztSYwf0OXaJ8Eaqr-3W9vQ76CltJb8OFZhMITf88Ng5OdSTMPrzJx5AvwK4sUv-C77MjaSwufoxZspHbbM-fD4O8oueIbLof3MGBIdNuDqKyOdOY_CvcvZZ3vQ6UgMLX_AhRG2rd/s72-c/hopeW.jpg
DIMBWI LA HABARI TZ
https://dimbwilahabari.blogspot.com/2017/07/usikatishwe-tamaa-kwa-kukataliwa-na.html
https://dimbwilahabari.blogspot.com/
https://dimbwilahabari.blogspot.com/
https://dimbwilahabari.blogspot.com/2017/07/usikatishwe-tamaa-kwa-kukataliwa-na.html
true
8218800783604508792
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago