post-feature-image
HomeHABARI

Aingia matatani baada ya kupulizia wenzake kemikali usoni

  Thursday, July 27, 2017   MADALALI wanne wa madini ya Tanzanite (mawe), wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuwaumiza m...

Haya ndiyo Maajabu 6 ya Dunia
Pwani: Mwanamke auawa, Polisi watangaza vita!
Tangazo la nafasi za kazi 3,152 kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.


MADALALI wanne wa madini ya Tanzanite (mawe), wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuwaumiza macho kwa kemikali aina ya ‘pepper spray’ baada ya kutofautiana malipo na madalali wenzao waliowauzia madini hayo.

Habari kutoka polisi zilithibitisha jana kuwashikilia madalali hao, Schola Mwanga, Margareth Mushi, Sued Mwanga na Dorice Mushi, kwa tuhuma za kufanya kitendo hicho.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Charles Mkumbo hakuweza kupatikana kutoa ufafanuzi zaidi.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufani ya Mkoa ya Mount Meru, Dk. Jackline Urio, alithibitisha kupokea wagonjwa watano ambao alisema uchunguzi unaendelea kujua walimwagiwa aina gani ya kemikali.

Alisema kutokana na hali zao, wagonjwa hao walitarajiwa kuhamishiwa Hospitali ya Rufani ya KCMC ya mkoani Kilimanjaro, jana.

Alisema waliojeruhiwa walikuwa katika biashara ya madini na wakaletwa hapa wakilalamika macho yanauma, wakapewa huduma ya kwanza ya kuwaosha macho kwa kushauriana na madaktari bingwa wa macho wa Dar es Salaam.

Aliwataja wagonjwa hao kuwa ni Sabas Laizer, Lucas Soto, George Nyakila, Moringe Mollel na Ngalama Mapena.

Alisema watu hao walidai kumwagiwa ‘spray’ kwenye macho, majira ya saa 10 na walianza kufikishwa hospitalini hapo mmoja mmoja kuanzia saa 12 jioni.

"Lakini kwa sasa tunawahamishia hospitali ya KCMC kwa sababu kule kuna madaktari bingwa wa macho, watachunguzwa vizuri kujua madhara waliyopata," alisema.

Wakizungumzia tukio hilo lililotokea mtaa wa Pangani jijini hapa, baadhi ya watu walioshuhudia, walidai madalali hao walitaka walipwe fedha (kamisheni) ya kuwauzia mawe hayo.

Lakili walisema madalali waliopewa mawe hayo kuuza walishindwa kuwapa fedha hizo kwa kile walichodai walikuwa bado hawajalipwa.

Walisema hali hiyo ilizua kutoelewana kati yao kiasi cha kuzua ugomvi na ndipo dalali mmoja alipoingia ndani ya gari na kuchukua ‘pepper spray’ na kuwapulizia usoni.

“Pepper spray’ ni aina ya kemikali inayowekwa katika kopo maalum mithili ya dawa ya mbu na ikipulizwa usoni kwa mtu inaumiza macho yake na kuyafanya yasione kwa muda.

Katibu wa Chama cha Madakali mkoani hapa, Noel Olovaroya, alisema tukio hilo lilitokea baada ya kutofautiana katika masuala ya biashara.

Alishukuru daktari bingwa wa hospitali hiyo kwa kuwashughulikia vizuri wagonjwa hao na kuomba serikali kuongeza madaktari wa macho katika hospitali hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya madalali wenzake, waliojeruhiwa, Ngalama Mapena ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Madalali wa Madini, alisema chanzo cha tukio hilo ni yeye aliuziwa madini ya Tanzanite na dalali mmoja kwa Sh milioni 3.2 na makubaliano yalikuwa angemlipa kesho yake (juzi)  ambayo ndio siku ya tukio.

"Lakini nikiwa pale baada ya kujibu hivyo nikaona gari RAV 4 rangi nyeusi, wakashuka wanawake wawili ambapo mmoja namfahamu akanipulizia kitu kama perfume usoni na huku akitukana na ghafla nikapoteza fahamu," alisema.
Alisema mwanamke huyo ni dalali mwenzake.
Name

BURUDANI HABARI MAKALA MICHEZO
false
ltr
item
DIMBWI LA HABARI TZ: Aingia matatani baada ya kupulizia wenzake kemikali usoni
Aingia matatani baada ya kupulizia wenzake kemikali usoni
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgQgm8uh6PnIyXx4df38-t_yUyfaozjNZ7677raTThyMfyBE1CL7ql6tuLce2RvLBiPR6SmlNMn7cbTGdV1-kjmfnR3gGHr3HssGjRy9gZtt6i7FDzubAdUs90M17-r6cWDW9mwYBqnpk8/s400/bad+news.webp
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgQgm8uh6PnIyXx4df38-t_yUyfaozjNZ7677raTThyMfyBE1CL7ql6tuLce2RvLBiPR6SmlNMn7cbTGdV1-kjmfnR3gGHr3HssGjRy9gZtt6i7FDzubAdUs90M17-r6cWDW9mwYBqnpk8/s72-c/bad+news.webp
DIMBWI LA HABARI TZ
https://dimbwilahabari.blogspot.com/2017/07/aingia-matatani-baada-ya-kupulizia.html
https://dimbwilahabari.blogspot.com/
https://dimbwilahabari.blogspot.com/
https://dimbwilahabari.blogspot.com/2017/07/aingia-matatani-baada-ya-kupulizia.html
true
8218800783604508792
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago