Trump na Merkel waongoza kumbukumbu za mshindi wa tuzo ya Nobel Liu Xiaobo 14 july 2017 Hivi ni viunganisho vya nje na vitafungua kat...
Trump na Merkel waongoza kumbukumbu za mshindi wa tuzo ya Nobel Liu Xiaobo
Rais Trump na kansela wa Ujerumani Angela Merkel wameongoza kumbukumbu za mchina aliyeshinda tuzo ya amani ya Nobel Liu Xiaobo, ayelikufa kutokana na saratani ya ini.

Hata hivyo, serikali ya Beijing ambayo ilimhukumu kifungo cha miaka kumi jela kwa tuhuma za kutaka kupindua serikali haijatambua kifo chake.

Mpaka sasa taarifa ya kifo chake haijatajwa katika vyombo vya habari vya nchi hiyo, huku taarifa kutoka vyombo vya kimataifa zikichujwa nchini China.
Merkel amesifu ujasiri wa Liu Xiaobo huku Trump nae akisema amesikitishwa na taarifa za kifo cha mtu ambae alijitolea maisha yake kwa ajili ya demokrasia